Tuesday, January 31, 2012

MUHESHIMIWA MWAKYEMBE VIPI HIZO SWAGGA ZA MIKONONI DAR ES SALAAM BARIDI KALI SANA?

Naibu waziri wa ujenzi na mbemge wa kyela mkoani mbeya Dr.Harrison Mwakyembe,akitoka kanisani kawe jijini Dar es salaam akiwa ametupia swagga flani mikononi ambazo nchi za baridi uvaa kwa ajili ya kujizuia baridi isiwapate mikononi.

TABIA YA MASTAA KUTEMBEA BILA YAKUVAA NGUO YA NDANI YAMTIA AIBU CRISTINA AGUILERA

                               UKIMTAZAMA MIGUUNI UTAJUA AIBU GANI IMEMKUTA

          NADHANI INAWEZA KUWA FUNDISHO KWA WENYE TABIA HII

MKASI NA STEVE NYERERE

Sunday, January 29, 2012

POOL TABLE

WEMA SEPETU AWAFUNGUKIA MASHAROBARO UHARO.

Hatimaye mrembo na msanii Wema Sepetu, ameweka wazi kuwa hataki tena kutembea na masharobaro kwani mapenzi yao yanakuwa hayana malengo zaidi ya kuchezeana.

Akizungumza hivi karibuni msanii huyu alisema kuwa msanii anayemfananisha na sharobaro ni aliyekuwa mpenzi wake
Nassib Abdul ‘Diamond’, kwani endapo angekuwa hayuko hivyo basi anaamini mapenzi yao yangedumu kwa muda mrefu.

Alisema kwa sasa anahitaji kutoka na mwanaume aliyemzidi umri kwani anaamini watu hao wanakuwa na mapenzi ya dhati tena hawana wivu kama watoto wadogo ambao muda wote hupenda kuwa karibu na wapenzi wao badala ya kufanya kazi.


“Kila kitu kina muelekeo wake, mapenzi yangu mimi na Diamond yangeweza kudumu lakini kutokana na usharobaro alionao ndiyo uliosababisha yote yaliyotokea, na ndiyo maana nasema kwamba ni bora kutembea na mwanaume aliyekuzidi umri mnaweza kufika mbali,”
alisema.

Msanii huyu alisema hata hivyo ni bora afunge ndoa na mwanaume atakayempata ambaye anajua maana ya mapenzi kuliko kutembea na vijana wadogo ambao hawajui nini maana ya mapenzi na hawana muelekeo wa maisha

HUSSEIN MACHOZI-JELA

Friday, January 27, 2012

SAMAKI MKUNJE ANGALI MBICHI



AZRA MTOTO ALIEZALIWA MAHABUSU NA ANAENDELEA KULELEWA MAHABUSU KWA KOSA LA WAZAZI WAKE KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA.

 AZRA MTOTO ALIEZALIWA MAHABUSU MBEYA AKIONEKANA MWENYE AFYA NJEMA.
 MAMA NA BABA AZRA WATUHUMIWA WA KESI YA MADAWA YA KULEVYA WAKIWA NA MTOTO WAO KATIKA MAHABUSU YA MAHAKAMA KUU MBEYA ENEO AMBALO WAZAZI WAKE WALIKAMATWA NA SHEHENA YA DAWA ZA KULEVYA ZENYE THAMANI YA BILLIONI 1.2
GARI YA WAZAZI WA AZRA ILIOTUMIKA KUHIFADHIWA MADAWA HAYO YA KULEVYA AMBAYO WALIKAMATWA NAYO TUNDUMA MKOANI MBEYA MPAKA WA TANZANIA NA ZAMBIA.


Wakati Tanzania ikiwa imeridhia mkataba wa kimataifa wa kutekeleza na kulinda haki za watoto na kusimamia kwa karibu ulinzi wa haki za binadamu, sasa serikali ina kila sababu ya kuangalia haki za watoto walioko gerezani kwa makosa ya wazazi wao.
  Miongoni mwa haki ambazo serikali inapaswa kuchunguza kwa undani na kubainisha kisa kilichosababisha mtoto mdogo wa kike wa miezi sita , Azra Vuyo Jack, ajikute yeye na wazazi wake wakiwa katika mahabusu ya gereza la Ruanda jijini Mbeya wakikabiliwa na tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya.
  Azra ambaye kwa jina la utani, kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na Mbeya yetu huko gerezani anaitwa Merryciana au bibi jela jina ambalo limezoeleka zaidi mbali ya jina lake halisi alilopewa na wazazi wake la Azra   .
   Mtoto huyo wa kike aliendelea kukua katika tumbo la mama yake akiwa gerezani, hatimaye alizaliwa salama Julai 15 mwaka jana katika hospitali ya wazazi meta.
  Mama yake ni Anastazia Cloete (27) mwenye asili ya kizungu, raia wa Afrika ya kusini
  Cloete alikamatwa mwaka juzi, Novemba katika mpaka wa Tanzania na Zambia , mji mdogo wa Tunduma akiwa mjamzito na kutupwa mahabusu katika gereza hilo hali iliyomfanya aendelee  kulea ujauzito wake.
  Uchunguzi wa kina uliendelea kufanywa na madaktari wa hospitali hiyo hadi alipojifungua salama.
   Uchunguzi wa tukio la mtoto huyo hadi sasa umezusha mwendelezo wa harakati za kihabari na wanaharakati wa haki za binadamu kuona umuhimu wa kuondolewa kwa mtoto huyo ambaye kwa muda wote tangu azaliwe amekuwa akitumia maziwa ya kopo na hanyonyeshwi na mama yake mzazi.
  Mmoja wa ya wasamaria wema aliyejitolea kuwahudumia watuhumiwa hao waliyokumbwa na tuhuma za kukutwa na dawa hizo ni Emily Mwaituka ambaye amekuwa akifanya kazi kubwa ili kuhakikisha mtpto anakuwa na afya nzuri kwa kununuliwa makopo mawili ya maziwa kila wiki tangu alipozaliwa julai, mwaka jana.
  Mwaituka anasema amekuwa akinunua kopo moja la maziwa ya unga aina ya SMA 1 ambalo huuzwa sh 26000 na anapaswa kununua makopo mawili ili kuweza kumudu mahitaji ya mtoto huyo wa kike ambaye hanyonyi maziwa ya mama yake mzazi anayesubiri hatima ya kesi inayomkabili akiendelea kuwa mahabusu kwenye gereza la Ruanda jijini Mbeya.
  Uchunguzi uliofanywa na Mbeya yetu  umegundua kuwa Cloete aliyekuwa akisoma nchini kwao katika chuo cha Capetech alijifungua mtoto wa kike miezi sita iliyopita baada ya kushikwa uchungu akiwa mahabusu na kukimbizwa hospitali ya wazazi ya meta.
  Cloete ambaye amekuwa akitumia majina mawili kwani alipolazwa katika hospitali hiyo aliandikishwa jina la Anastazia Elizabeth wakati alifikishwa hospitalini hapo kwa uchunguzi akiwa mjamzito Januari 14 mwaka jana na kufunguliwa jarada la matibabu lenye namba 46 – 26 – 83.
  Uchunguzi umebaini kuwa raia huyo wa afrika ya kusini na mumewe , Vuyo Jack ( 31 ) waliokamatwa mpakani hapo, aligundulika kuwa mjamzito alipokuwa mahabusu na kuanza kupatiwa matibabu sahihi yaliyosaidia ujauzito wake kukua vizuri.
  Habari za ndani zinadai kuwa kwa muda wote huo baada ya ujauzito wake kugundulika alikuwa akipatiwa matibabu chini ya uangalizi wa madaktari na alipofikia  hatua za mwisho mjadala mzito ulifanywa na jopo la madaktari walioonyesha mashaka kuwa asingeweza kujifungua kwa njia ya kawaida na kutakiwa afanyiwe upasuaji.
 Imeelezwa kuwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake katika hospitali hiyo Peter Msafiri , alipofanya uchunguzi alibaini kuwa raia huyo hapaswi kufanyiwa upasuaji kwa vile alikuwa na uwezo wa kujifungua bila matatizo.
  Dk Msafiri alipohojiwa anasema Cloete alijifungua salama ingawa walitaka kumfanyia upasuaji lakini alipinga hatua hiyo na kudai kuwa anaweza kujifungua salama kwa njia ya kawaida.
  Baadhi ya wauguzi wa hospitali hiyo ambao hawakutaka majina yao kutajwa walidai kuwa raia huyo wa Afrika ya Kusini alijifungua mtoto wa kike na kwamba mama yake akiwa mahabusu amekataa kumyonyesha kwa madai kuwa hapati mlo wa kutosha unaomuwezesha kutoa maziwa ya kutosha kwa ajili ya mwanae.
  Cloete alilazwa hapo kwa ajili ya uchunguzi , hamnyonyeshi mtoto wake, kweli amejifungua mtoto mzuri wa kike, amesema kuwa hawezi kumnyonyesha na  anamlisha maziwa ya kopo akidai kuwa akinyonyesha atakosa nguvu kwa kuwa mahabusu alikowekwa hapati lishe bora anadai muuguzi mmoja.
 Miongoni mwa wanaharakati wa haki za binadamu walioguswa na habari za mtoto huyo kuendelea kukaa mahabusu na mama yake kulimgusa. Mchungaji William Mwamalanga, anasema kuwa kitendo cha mtoto huyo kuishi katika mazingira hayo hakuendani na haki za binadamu ambazo Tanzania imeridhia kwenye umoja wa mataifa.
  Mwamalanga anasema yeye na wanaharakati wenzake wanaandaa mpango maalumu wa kupigania haki ya mtoto huyo na kuhakikisha kuwa anaondolewa mahabusu baada ya kubainika kuwa amekuwa hanyonyeshwi na mama yake mzazi tangu alipozaliwa kwa madai kuwa hawezi kumnyonyesha kutokana na lishe duni anayopata akiwa mahabusu.
  Nakushukuru sana kuzisoma taarifa hizi, tunajiandaa ili kuona njia sahihi inayoweza kutusaidia kumtoa mtoto huyo mahabusu na kuiomba serikali iangalie kwa undani shauri hili kupitia kwa mwendesha mashtaka mkuu wa serikali ili kujua haki na stahili za mtoto huyo mchanga vinginevyo tunakiuka haki za watoto na binadamu ambazo Tanzania imeridhia kuzitekeleza, anasema Mwamalanga.
  Kumbukumbu za tukio hilo tulizonazo zinaonyesha kuwa raia hao wawili wa Afrika ya Kusini, waliokuwa wakiishi mtaa wa 2A Valley Road – Schaapkraal – Capetown walikamatwa na kilo 42 .5 za dawa za kulevya Novemba 18 mwaka juzi katika mpaka wa Tunduma na kufunguliwa – jalada namba TDM/IR/1763/2010.
  Katika tukio hilo ambalo Vuyo na Cloete walinaswa na dawa hizo walizozificha kwenye gari aina ya Nissana Hard body yenye namba za usajili CA – 508 – 656 lililokuwa likimilikiwa na Vuyo Jack waliokuwa wakitokea mkoani Morogoro kuelekea Afrika ya Kusini, Cloete alikuwa akisoma katika chuo cha Capetech.
  Kwa mujibu wa taarifa za ndani ambazo zimethibitishwa na Mkemia Mkuu wa Serikali dawa hizo za kulevya ni paketi 26 za cocaine zenye uzito wa kilo 28.5 paketi tatu za Heroine zenye uzito wa kilo 3.25 na paketi nane aina ya Morphine zenye uzito wa kilo 3.25, madawa hayo yote yanathamani ya zaidi ya sh bilioni 1.2.
HABARI KWA HISANI YA MBEYA YETU.

Wednesday, January 25, 2012

DAR WAKILIA NA JOTO SWEDEN NAO KWA BARIDI

                       Sidhani kama kuna kwenda kujenga taifa leo gari yote imefunikwa

                                 Njia ya kupita na miguu nayo imebidi snow isogezwe
                                 Uwanja wa mpira wa kikapu hauchezeki kwa sasa
                                 Nilipoamka kwenda kibaruani hali niliikuta hvi hatari.
 Sehemu kama hii kipindi cha joto viti vyote vinajaa hapa kijiweni lakini wakati huu kila mtu anapakimbia.
                                   Kiatu hiiiiiiiicho kinaishia ndani ya barafu.

UKIWA NJE NYUMBA NDANI UNAKUTANA NA MAUZO YA NGUO DUKA JIPYA STOCKHOLM


                       Nje ya duka unakutana na kijiwe samli unaweza kupumzika

AFUNGA NDOA NA MAITI YA MCHUMBA WAKE KABLA YA KUZIKWA.

 Mkurugenzi ktk kituo cha televisheni moja nchini Thailand Chadil Deffy aamua kuonyesha upendo wake wa dhati kwa mchumba wake serinya baada ya kifo chake.
Jamaa alichukua jukumu la kumuoa mchumba wake akiwa tayari maiti,alieleza kwa uma aliamua kufanya tukio hilo kwa kua walishapanga na mchumba wake huyo wa siku nyingi waoane kwa bahati mbaya akapata ajali na kufariki.Baada ya kufunga nae ndoa mchumba wake kitendo kilichofata ni kumzika mke wake huyo.Jamaa aliamua kusambaza picha katika mtandao wa facebook na youtube.

DOGO HAMIDU FT MR.BLUE &YUNG D-NIMEKASIRIKA

MAITI IMEBEBWA KATIKA PIKIPIKI BUKOBA,SIJUI NANI WA KULAUMIWA KWA HILI.

 Dereva wa pikipiki aliebeba maiti huko mkoani nukoba akiwa ktk mapumziko kabla ya kuendelea na safari yke.
Kiukweli inasikitisha na niukiukwaji wa haki za binadam na sijui nani alaumiwe hapa maana kweli kuna sehem kubwa ya nchi yetu Tanzania watu maskini sana.Kama ujioneavyo maiti inavyodhalilishwa kwa kubebwa katika piki piki na kufungwa na mipira kama mzigo wa kuni.Hivi leo hii tupo karne ya 21 na mambo bambo si shwari nchi yetu sijui nani wa kumtupia lawama.

WAETHIOPIA WALIOINGIA TANZANIA KINYUME CHA SHERIA WAKAMATWA NA UAMIAJI MOROGORO

 Hapa wakishuka katika gari kuelekea mahakamani kusoemwa mashitaka yao watuhumiwa hao wapatao 97.
Raia wa ethiopia wakiwa chini ya ulinzi baada ya kukamatwa kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria.
    kwa hisani ya kajuson.

Monday, January 23, 2012

MFALME YUSUFU AWAKILISHA VYEMA JAHAZI NDANI YA USA

 Mzee Yusufu kiongozi wa kundi la Jahazi alilifikisha vyema jahazi nchini usa na kupagawisha mashabiki wote walioudhulia katika onyesho hilo.Mzee yusuf japo alifika usa peke yke bila kundi lake lakini kazini alioifanya ni sawa kabisa hakuna aliejua kama amekwenda kutoa burudani peke yke.

                                                                Vidole vidole
                                  Mzuka uliwapanda kisawa sawa wakazi wa usa
                               Vidole juu vilinyooshwa kisawa sawa burudani ilipofika mahala pake
                                   Mfalme Yusufu akicheza sambamba na mashabiki wake

Saturday, January 21, 2012

ANAHITAJI MSAADA WAKO MDAU ILI APONE

 Mtoto Josephat mwenye umri wa miaka 16 ana tatizo la uvimbe mkubwa kwenye jicho ambao umetunga usaha na kumsababishia kutoona kabisa kwani kila anavyozidi kukua na uvimbe huo unazidi kuongezeka.


Kwa mujibu wa maelezo yake Josephat amesema tatizo hilo limemuanza tangu akiwa mtoto na hajawahi kupatiwa msaada wowote kwasababu hana ndugu wala mahali pa kuishi na sasa hivi ana tangatanga mitaani baada ya kutoka Dodoma alipokuwa akiishi katika kituo cha basi.
Mtoto huyu amefika leo mchana katika Ofisi EATV/EA Radio akiomba msaada wa matibabu kuhusiana na tatizo hilo ambalo hajui hatma yake itakuwa nini na kiukweli nimejisikia vibaya sana kwani hali yake ni mbaya sana huwezi kumuangalia mara mbili au hata mara moja kama una roho nyepesi tafadhali kama una uwezo msaada wako ni muhimu sana kwakuwa yeye mwenyewe hakupenda ni mipango ya Mungu,Hapo alipo hajui atakula nini wala atalala wapi.TUSAIDIANE!!!


Kama umeguswa na hali ya mtoto huyu na unahitaji kumsaidia kwa njia yoyote ile,Tafadhali tuwasiliane kupitia email marygorethrichard@gmail.com.


Kutoka kwa Dada marygoreth Richard.

Thursday, January 19, 2012

RAISI KIKWETE AONGOZA WANANCHI KATIKA MAZISHI YA REGIA MTEMA YALIOFANYIKA KILOMBERO MOROGORO

 Mweshimiwa raisi kikwete akiweka shahada la maua ktk kabuli la Regia Mtema,mbuge wa viti maalum kwa tiketi ya chadema.
                                  Raisi Kikwete akiweka mchanga ktk kabuli la Regia Mtema
Mamia ya wananchi wa Kilombero walioudhuria mazishi ya Regia Mtema wakiwa ktk majonzi makubwa kwa kuondokewa na mtu wao.

Tuesday, January 17, 2012

KADA WA CCM ALIYEMWAGIWA TINDIKALI IGUNGA AREJEA NCHINI BAADA YA MATIBABU NCHINI INDIA

MKAZI wa Igunga, Kada wa CCM, Mussa Tesha aliyekuwa nchini India kwa matibabu baada ya kumwagiwa tindikali usoni na watu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADAEMA), wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo jimboni humo (Igunga) mwaka jana, akizungumza na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam, baada ya kurejea nchini. Kulia ni Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha Mwigulu Nchemba ambaye alikuwa Meneja wa Kampeni za CCM jimboni humo.

DARLIVE YAZIDI KUPAMBA MBOTO KTK BURUDANI ZA KILA AINA

                                   Mkata nyonga wa tot akiwajibika jukwaani
 Malkia wa mipasho Tanzania Khadija Kopa na kundi zima la tot wakiwajibika ktk ukumbi wa darlive mbagala.
                                              Madee na tiptop nao walikuwepo
                 Umati wa watu ulioudhulia kiota hicho cha maraha kilichopo mbagala wakila bata

MAMIA WAUAGA MWILI WA MAREHEM REGINA MTEMA KTK VIWANJA VYA KARIMJEE DSM

Marehemu Regia Mtema mbunge wa viti maalum kwa tiket ya chadema enzi za uhai wake akiwa maeneo ya bunge dodoma.
 Makamu wa raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania DKT.BILAL akiaga mwili wa marehem Regia Mtema.
         Mwili wa marehem Regia Mtema ukipelekwa sehem maalum kwa ajili ya kuagwa na wananchi

Spika wa bunge la jamuhuri wa muungano wa Tanzania Anne Makinda akitoa rambi rambi na wasifa wa marehem kwa niaba ya bunge la Tanzania.

BABU TALE WA TIPTOP CONNECTIONS AANDAMWA NA STORY ZA UCHAWI

 Meneja wa kundi la tiptop conection babu tale leo amezungumzia tuhuma zilizoenea kuhusu yeye kwamba ni MCHAWI, stori ambazo zimeandikwa na mitandao mbalimbali.


Moja kati ya mitandao hiyo, umeamplfy kwamba boss huyo wa Tip top connection ni mchawi na huwa anatembea na kibegi chake flani, hakiachi hata awe anaenda, ambapo ukichunguza utagundua kwamba msanii yoyote atakayeingia tiptop connection alaf akaondoka baadae, ndo unakuwa mwisho wa career yake, yaaani lazima apotee kwenye muziki hata kama atajitahidi vipi, mfano ni kwa MB DOGG, PNC, Z ANTO, PINGU, KEISHA na sasa KASSIM ambae ameondoka juzijuzi lakini bado anasikika kiaina ila inasemekana muda c mrefu atachuja
              Kibegi anachotembea nacho babu tale kinachosadikiwa ndio uchawi wote unapatikana humu.

kwa kujibu, Babtale amesema “kuna mambo mengi nafanya mazuri lakini watu hawayaoni, kibegi changu nakitumia kuhifadhi vitu vyangu, kuna laptop na vitu vingine ninavyohifadhi, mtu anaponiandika kwamba Tale mchawi amempoteza msanii huyu, amemdidimiza msanii huyu, wnaashindwa kuelewa kwamba mwanzo mimi ndio nilifanya huyo msanii anga’e, na akiondoka kuwa chini yangu wengi wanafeli kwa sababu hawana MANAGEMENT nzuri”



Babtale anaeongoza TIPTOP CONNECTION iliyotimiza miaka 10 mwishoni mwa mwaka jana, ameongeza kwamba “kuna mambo mengi nafanya lakini hakuna anaesifia, mimi na Said Fela wa TMK family ndio tunamsimamia DIAMOND sasa hivi, tumemrudisha Ferooz na mchiriku wake, tumemrudisha SUMALEE lakini hakuna anae tusifia, watanzania hawakusifii mpaka Ufe, sio kitu kizuri” – BabTale